Ligi kuu ya England ni moja ya Ligi kubwa sana Duniani, Hizi ni point za kila timu katika misimu kumi.Manchester United imekaa kileleni mwa jedwali hilo na shukurani zimwendee Sir Alex Ferguson.Hata hivyo Chelsea wapo nyuma kwa pointi moja tu.Tangu kustaafu kwa Sir Alex Ferguson majira ya kiangazi mwaka 2013, Man United imekuwa na wakati mgumu katika michuano ya ligi kuu England na imemaliza nafasi mbili mbovu yaani nafasi ya 7 chini ya David Moyes na 4 ikiongozwa na Louis van Gaal.Licha ya matokeo hayo, mashetani hao wekundu wameongoza jedwali hilo, huku Arsenal wakishika nafasi ya 3 na Liverpool wakishika nafasi ya 4.


0 comments:
Post a Comment