TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA ILI UPATE MAFANIKIO KWA HARAKA ZAIDI

TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA ILI UPATE MAFANIKIO KWA HARAKA ZAIDI
Home » » Floyd Mayweather amchagua huyu, Game yake ya mwisho.

Floyd Mayweather amchagua huyu, Game yake ya mwisho.

                                    

Mashabiki wengi wa ndondi duniani bado wanahamu ya kutaka kujua je ni mwanamasumbwi gani atapambana na mkali wa mchezo huo kutoka marekani Floyd Mayweather ambapo hilo ndilo litakua pambano la mwisho kwa Floyd mayweather kwani baada ya hapo anastaafu rasmi kucheza mchezo huo.
Floyd Maywether pambano lililopita alimtwanga Mphilipino Manny Pacquayo ambapo baada ya hapo tetesi zilizagaa kwamba wawili hao wanaweza kurudiana kwenye mpambano wa mwisho wa Mayweather.
Lakini uvumi huo ulipotea ghafla mara baada ya kujitokeza kwa bondia Amir Khan ambaye alisema yupo tayari kupambana na Maywether kwenye pambano lake la mwisho.
Ukimya ulizidi kwani hakuna lolote lililoendelea na kuonyesha kwamba Amiri Khan atapigana na Maywether.
Lakini habari zilizovuja hapo jana ni kwamba Floyd Maywether ameamuakumchagua bondia De La Hoya ili apigane nae kwenye pambano lake la mwisho hapo mwezi septemba.
Endapo mambo yakiwa sawa, basi wawili hawa watakua wanarudiana kwani walishawahi kupigana mwaka 2007 na Floyd maywether aliweza kuibuka na ushindi wa point.
De La Hoya a.k.a The Golden Boy ni raia wa amerika na tayari ameshapigana mapambano 39, akishinda jumla ya 36 huku 30 yote akishinda kwa KO
 
 
Share this video :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Creating Website | WILLE Template | GOOGLE
Copyright © 2013. Dj Wille Zedon - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger